Baba Askofu Dkt Alex G. Malasusa (Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani )kulia na kushoto ni Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Askofo CHEDIEL Elinanza Sendoro kwa pamoja walishirikiana kuongoza ibada ya uzinduzi wa Ofisi ya Makao Makuu ya Dayosisi ya Mwanga. Ambayo yamezinduliwa siku ya Bwana ya Watakatifu wote. Sambamba na uzinduzi huo Kulikuwa na ibada maalumu ya kubariki Wachungaji sita wa Dayosisi ya Mwanga, Same na Karagwe pamoja na ibada ya shukrani kwa Dayosisi ya Mwanga kutimiza miaka sita toka kuanzishwa kwake
Copyright © 2021 - All Rights Reserved - Mwanga Diocese (ELCT.MWD)